Pakistan Imefikia Kiwango Duni Kwa Mara Nyingine.

Katika hatua ambayo si ya kawaida, uongozi wa Pakistani kwanzia kwa Rais wake hadi Waziri wa Mambo ya nje, walitoa maoni yao juu ya jambo ambalo ni la ndani kabisa kwa India. Katika Uamuzi usiopingwa uliotolewa na benchi la jaji watano la Mahakama Kuu ya India mnamo 9 Novemba, 2019, uliutatua mzozo wa zamani wa miliki ya ardhi ya Ayodhya huko Uttar Pradesh kwa ujenzi wa hekalu la Ram. Hii imekaribishwa sana na sehemu zote za jamii. Benchi pia ilitenga ekari tano za ardhi katika eneo maarufu huko Ayodhya ili kutambuliwa na serikali ya Muungano na serikali ya jimbo kwa ujenzi wa Msikiti. Ardhi hio ambayo inapiginiwa inafaa kubaki na kundi la wadhamini ambalo

linafaa kuundwa na serikali ya Muungano ndani ya miezi mitatu.

Utatuzi wa miliki ya ardhi huko Ayodhya umekaribishwa na vyama vyote kwenye mzozo. Akielezea kuridhika kwake kubwa na uamuzi huo, Waziri Mkuu Narendra Modi katika hotuba yake kwa taifa, jioni hiyo alisema jinsi ambavyo kila sehemu ya jamii ya India, kila jumuiya, watu wa kila dini, taifa zima wamekubali uamuzi huo na moyo wazi ni dhihirisho la maadili za kitamaduni za zamani za India, tamaduni, mila na roho yake asili ya udugu na maelewano.

Pakistan, hata hivyo ilitoa maoni isiyohitajika wala kuwa na maana juu ya uamuzi uliliotolewa bila kupingwa juu ya mzozo wa miliki wa ardhi ya Ayodhya. New Delhi hawakurejelea tu kwa mara moja maoni yaliyotolewa na Pakistan lakini pia walishutuma kwa vikali miundo maovu ya Islamabad. Wizara ya Mambo ya nje ya India katika taarifa ilisema, 'Ukosefu wa uelewa wa Pakistan haushangazi kwani ni kulazimishwa kwao kutoa maoni juu ya mambo ya ndani ya India kwa kusudi la wazi la kueneza chuki, ndiyo inashutumiwa sana'. Ikijibu taarifa ya Ofisi ya Mambo ya nje ya Pakistan na maoni ya Waziri wake wa Mambo ya nje, Shah Mahmood Qureshi, Wizara ya Mambo ya nje ilisema, India inakataa kabisa maoni yasiyohitajika na ya uwongo juu ya uamuzi wa Mahakama Kuu juu ya suala la kiraia ambalo linahusika kabisa na ndani ya India na linahusu kuzingatiwa kwa sheria na heshima sawa kwa imani zote na dhana ambazo sio sehemu ya maadili ya Pakistan.

Ilikuwa pia bahati mbaya sana kwamba Pakistan ilichagua kutoa maoni juu ya hali ya Kashmir na uamuzi wa Mahakama Kuu juu ya Ayodhya katika hafla ya uzinduzi wa Ukanda wa Kartarpur inayounganisha maeneo ya kuabudu mbili za kihistoria zinazojulikana zaidi, Dera Baba Nanak katika mkoa wa Gurdaspur wa Punjab nchini India na Gurdwara Darbar Sahib huko Kartarpur katika mkoa wa Narowal wa Pakistan. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa ukanda wa Kartarpur kwa upande wa India, Waziri Mkuu Modi alimpongeza Waziri Mkuu wa Pakistan Imran Khan kwa uelewa wake na heshima yake kwa hisia za Wahindi.

Walakini, viongozi wa Pakistani walichagua kuzua suala ya Kashmir na Ayodhya kwenye hafla hiyo kwa upande wao. Mahusiano kati ya India na Pakistan yameganda tangu shambulio la kigaidi katika kambi ya jeshi la Uri mwaka wa 2016, yakizidishwa zaidi na majibu ya Pakistan kuhusu kufutwa kwa kifungu cha sheria cha 370, ikiunganisha Jammu na Kashmir kikamilifu na India. Walakini, fursa ya kupunguza baridi, inayotolewa na nia njema iliyotokana na ukanda wa Kartarpur ilipotea wakati Pakistan ilizidisha hali hiyo zaidi na maoni yake yasiyohitajika juu ya uamuzi wa Ayodhya.

Pakistan kwa sasa inakabiliwa na mzozo mzito wa uchumi na Imran Khan akitishia serikali yake na umahiri wake kuipeleka nchi nje ya shida. Maelfu ya wanaharakati wa Jamiat Ulema-e-Islam, JuI (F) wakiongozwa na Mkuu wake Fazlur Rehman walikuwa wamekusanyika katika Islamabad wakitaka kujiuzulu kwa Waziri Mkuu. Vyama vingine vya upinzaji pia viko kwenye mikono dhidi ya serikali ya Pakistani. Waziri Mkuu wa zamani wa chama cha Waziri Mkuu Nawaz Sharif PML (N) na familia yake wameishtumu serikali ya Pakistani kwa kujaribu kumaliza chama chao.

Kulingana na wachambuzi, Waziri Mkuu Imran Khan labda anaweka ushujaa wa anti-India kwa kiwango kikubwa ili kupotosha umakini wa watu kutoka kwa shida kubwa za nyumbani. Lakini, Pakistan lazima ieleweke kwamba uhusiano na India hauwezi kuboreka isipokuwa utaacha kuingiza uhasama na kuingilia maswala ya ndani ya India.

Comments

Popular posts from this blog

Mpango wa wazir mkuu wa India ,  unaoitwa Mann ki baat,  Maana yake ni maneno ya moyo, ambapo waziri mkuu wa India amehutubia watu wa taifa 

WAZIRI MKUU ANATOA WITO KWA AJILI YA KUWEKA MAPENZI YA TAIFA KWANZA

Kujiuzulu kwa Iran Kutoka JCPOA Na Matokeo yake Duniani.