Waziri Mkuu Ataka Makampuni Mapya Kuwa na Matarajio Makubwa.
Waziri Mkuu Narendra Modi alihutubia nchi kupitia mpango wake wa “Mann ki Baat” kupitia redio ya All India Radio. Katika toleo la 68 la Mann ki Baat, Waziri Mkuu alisema kuwa vijana walishiriki katika hafla ya Ubunifu wa aplikisheni ya ‘AatmaNirbhar Bharat’. Alibainisha kuwa karibu theluthi mbili ya washirika wa hafla hio walikuwa vijana kutoka miji yenye idadi ya watu wa katikati (miji ya daraja ya pili na tatu). Matuzo yamepewa aplikisheni karibu dazeni mbili katika vitengo tofauti, alisema. Aliwauliza wasikilizaji wa redio ya All India Radio kupata kujifahamisha na aplikisheni hizi na kuungana nazo. Waziri Mkuu alitaja aplikisheni hizi kadhaa, zikiwemo aplikisheni ya Kutuki Kids learning, aplikisheni ya watoto; aplikisheni ya jukwaa ndogo la kublogi au kuandika majarida inayoitwa ku KOO ku; Chingari App ambayo inakuwa maarufu kati ya vijana; aplikisheni ya ‘Ask Sarkar’ ambayo hupata habari sahihi juu ya miradi ya serikali na aplikisheni ya Step Set Go- fitness nk. ...