Bajeti ya Taifa Kuzingatia Ukuaji.
Bajeti ya Taifa ya 2020- 21 imefanya hatua ya maamuzi ya kuzuia kuporomoka kwa uchumi wa India na kuurejesha kwa kufunua hatua kadhaa. Hii ni kati ya kuweka pesa nyingi mifukoni mwa watu, kusaidia sekta ya kilimo kwa kuongeza mapato mara mbili ya wakulima na kuondolewa kwa ushuru wa gawio kwa makampuni ili kukuza biashara.
Kutunga bajeti katika nyakati za changamoto za kifedha ni kazi ngumu lakini, Waziri wa Fedha Bi Nirmala Sitaraman alifanya kitendo cha kusawazisha kwa kugawa nafasi za kutosha za matumizi ya rasilimali kwa kuhakikisha kwamba sehemu kubwa ya mkopo wa serikali itaenda kwa hii. Serikali kwa hivyo, ilionyesha jukumu lake katika miradi ya miundombinu zaidi juu ya uundaji wa mali isiyohamishika katika usafi wa mazingira na utunzaji wa maji kama sehemu ya lengo la jumla la kuleta Urahisi wa kuishi kwa kila mwananchi ili "kuruka hadi kiwango kingine cha afya, ustawi na uendelevu ”, kama bajeti ilivyoelezea vizuri.
Chini ya mradi wa 'Bomba la Miundombinu ya Kitaifa' la Rupia. karori 102 lakh iliyoenezwa kwa miaka mitano, jumla ya Rupia. karori 22,000 zilitengwa mwaka huu wa fedha kwa usawa wa kufadhili idadi ya makampuni ya fedha ya infra. Hii itasaidia kuyainua mara kadhaa na kupanua fedha zinazohitajika kwa muda mrefu kwa miradi ya infra.
Kama hatua za misaada zinazohitajika kwa sekta halisi za uchumi husika, kupotoka kutoka kwa Sheria ya Usimamizi wa Bajeti na majukumu ya fedha (FRBM), upungufu wa fedha wa 2019-20 ungepita lengo la asilimia 3.3 ya Pato la Taifa kwa asilimia 3.8. Ongezeko huu wa asilimia 0.5 unathibitishwa kwa sababu uchumi mzuri kama India hauwezi kupoteza kasi ya ukuaji yake. Bajeti ilitunza nambari ya upungufu endelevu ili kuhakikisha usawa wa kati ya vizazi katika usimamizi wa fedha.
Kati ya kitengo pana ya wadau wa uchumi, katika kilimo, unyunyuzi wa maji na maendeleo ya vijijini, mapendekezo mapya yanajumuisha ufadhili wa uwezo kwa uundaji wa maghala yanayofaa, makampuni ya usambazaji wa bidhaa zinazoharibika haraka ya taifa na utoaji wa juu wa mikopo ya kilimo wa Rupia. karori 15 lakh kwa mwaka wa fedha ujao. Mpango mkubwa wa elimu wa Rupia. karori 99,300 na karibu Rupia. karori 3200 ya maendeleo ya ustadi imetengwa katika mwaka ujao wa fedha.
Ili kuhakikisha kuwa watu wanabaki na mapato ya kutosha baada ya kupeana deni zao za ushuru, bajeti imekuja na enzi mpya ya ushuru iliyorahisishwa kama mbadala wa ile ya zamani(sans the plethora). Katika azma ya kumaliza mizozo ya ushuru na kuweka imani kwa walipa ushuru, mizozo ya madeni ya ushuru yanapaswa kulipwa, kiasi tu cha ushuru ndio kinapaswa kulipwa na riba na adhabu itatolewa kwa muda mfupi hadi Juni 2020. Ili kuleta utulivu kwa risiti kutoka kwa ushuru wa bidhaa na huduma (GST), GST iliyorahisishwa na mchakato wa fidia wa kiotomatiki utatekelezwa.
Kwa makampuni kukua hadi uwezo wao kamili, kiwango cha ushuru ya mapato halisi ya makampuni ya asilimia 15 kwa makampuni mapya ya ndani katika sekta ya utengenezaji kilichotangazwa Septemba iliyopita kitatolewa kwa sekta ya nguvu pia. Kwa Fedha za Hazina ya Juu (SwFs) ya serikali za nje na uwekezaji mwingine wa kigeni, makubaliano ya ushuru yatatolewa, wakati faida za ushuru zilizobaki kwa 'makampuni yanayoanza' (Start-Up) kwa njia ya kupunguzwa kwa asilimia 100 ya faida zao zinaimarishwa kwa kuongeza kiwango cha juu cha mauzo na kipindi cha kustahiki. Vitengo maalum vya miliki ya serikali vitafunguliwa kwa wawekezaji wasio wakaazi. Kiwango cha juu ya Jukwaa la Uwekezaji wa Kigeni (FPI) kwa vifungo vya mashirika kitaongezeka kutoka asilimia 9 hadi 15 ili kuimarisha soko la deni la ndani.
Bajeti imetoa kwa viwango vya kodi vya kawaida kwa mashirika na kuongezeka kwa kizingiti cha ukaguzi wa biashara ndogo ndogo na za kati ili kuhakikisha kuwa hakuna shida ya ushuru.
Serikali ina matumaini ya kuongeza rasilimali zaidi kufadhili mipango yake ya maendeleo zaidi kupitia uuzaji wa mali za kimkakati na lengo la kutowekeza kwa kiwango cha Rupia. karori 2.10 lakh katika mwaka ujao wa fedha, dhidi ya Rupia. karori 65,000 katika mwaka 2019-20. Bajeti ni mchanganyiko mzuri wa kupunguzwa kwa ushuru na uwekezaji kwa sehemu zenye manufaa kwa ajili ya kufufua ukuaji. Pato la msingi linalokadiriwa kwa mwaka unaofuata wa fedha ni asilimia 10.
Comments
Post a Comment